< Zaburi 12 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
למנצח על השמינית מזמור לדוד הושיעה יהוה כי גמר חסיד כי פסו אמונים מבני אדם׃
2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
שוא ידברו איש את רעהו שפת חלקות בלב ולב ידברו׃
3 Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
יכרת יהוה כל שפתי חלקות לשון מדברת גדלות׃
4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
אשר אמרו ללשננו נגביר שפתינו אתנו מי אדון לנו׃
5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, nitainuka sasa,” asema Bwana. “Nitawalinda kutokana na wale wenye nia mbaya juu yao.”
משד עניים מאנקת אביונים עתה אקום יאמר יהוה אשית בישע יפיח לו׃
6 Maneno ya Bwana ni safi, kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, iliyosafishwa mara saba.
אמרות יהוה אמרות טהרות כסף צרוף בעליל לארץ מזקק שבעתים׃
7 Ee Bwana, utatuweka salama na kutulinda na kizazi hiki milele.
אתה יהוה תשמרם תצרנו מן הדור זו לעולם׃
8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali wakati ambapo yule aliye mbaya sana ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
סביב רשעים יתהלכון כרם זלות לבני אדם׃

< Zaburi 12 >