< Zaburi 12 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
Help, Jehovah, for the holy man ceases, for the faithful fail from among the sons of men.
2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
They speak falsehood everyone with his neighbor. With flattering lip, and with a double heart, they speak.
3 Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
Jehovah will cut off all flattering lips, the tongue that speaks great things,
4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
who have said, With our tongue will we prevail. Our lips are our own. Who is lord over us?
5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, nitainuka sasa,” asema Bwana. “Nitawalinda kutokana na wale wenye nia mbaya juu yao.”
Because of the oppression of the poor, because of the sighing of the needy, now I will arise, says Jehovah. I will set him in the safety he gasps for.
6 Maneno ya Bwana ni safi, kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, iliyosafishwa mara saba.
The words of Jehovah are pure words, as silver tried in a furnace on the earth, purified seven times.
7 Ee Bwana, utatuweka salama na kutulinda na kizazi hiki milele.
Thou will keep them, O Jehovah. Thou will preserve them from this generation forever.
8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali wakati ambapo yule aliye mbaya sana ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
The wicked walk on every side when vileness is exalted among the sons of men.