< Zaburi 119 >

1 Heri wale walio waadilifu katika njia zao, wanaoenenda katika sheria ya Bwana.
Nowa dunu ilia da giadofasu mae hamone, Hina Gode Ea Hamoma: ne sia: i nabawane hamonanea, ilia da hahawane bagade.
2 Heri wale wanaozishika shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wao wote.
Nowa da ilia asigi dawa: su huluane amoga Hina Gode Ea hamoma: ne sia: i amoma noga: le fa: no bobogesea, ilia da hahawane bagade.
3 Wasiofanya lolote lililo baya, wanaoenenda katika njia zake.
Ilia da giadofasu hame dawa: Ilia da Hina Gode Ea logodafa, amoga ahoa.
4 Umetoa maagizo yako ili tuyatii kwa ukamilifu.
Hina Gode! Di da Dia hamoma: ne sia: i ninima ianu, amo mae yolele nabawane hamoma: ne sia: i dagoi.
5 Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara katika kuyatii maagizo yako!
Na da Dia hamoma: ne sia: i amo defele hamomusa: bagadewane hanai gala.
6 Hivyo mimi sitaaibishwa ninapozingatia amri zako zote.
Na da Dia sema amo noga: le nabawane hamosea, na da gogosiasu hame ba: mu.
7 Nitakusifu kwa moyo mnyofu ninapojifunza sheria zako za haki.
Na da Dia moloidafa fofada: su hou noga: le ado boba: lalea, na dogo da fofoloiba: le, na da Dima nodomu.
8 Nitayatii maagizo yako; usiniache kabisa.
Na da Dia hamoma: ne sia: i nabawane hamomu. Na maedafa yolesima!
9 Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani? Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.
Ayeligi da habodane ea esalusu fofoloiwane ouligima: bela: ? E da Dia hamoma: ne sia: i amo nabawane hamosea, ea esalusu da fofoloi ba: mu.
10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote, usiniache niende mbali na amri zako.
Na dogoga huluane, na da Dima fa: no bobogemusa: dawa: Na da Dia hamoma: ne sia: i amo na da giadofasa: besa: le, Dia na fidima.
11 Nimelificha neno lako moyoni mwangu ili nisikutende dhambi.
Na da Dia hamoma: ne sia: i amo na dogo ganodini dawa: i diala, amasea na da Dia hamoma: ne sia: i hame giadofale hamomu.
12 Sifa ni zako, Ee Bwana, nifundishe maagizo yako.
Hina Gode! Na da Dima nodone sia: sa. Dia noga: idafa hou nama olelema.
13 Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote zinazotoka katika kinywa chako.
Na da Dia hamoma: ne sia: i huluane nama i, amo eso huluane bu ha: giwane dabuasili adolalumu.
14 Ninafurahia kufuata sheria zako kama mtu afurahiaye mali nyingi.
Dia hamoma: ne sia: i amo na da nodone amo fawane baligili fa: no bobogesa. Na liligi bagade amo gagumusa: hame dawa: sa.
15 Ninatafakari maagizo yako na kuziangalia njia zako.
Na da Dia hamoma: ne sia: i amo dadawa: le bai hogosa. Na da Dia olelesu hou amo abodesa.
16 Ninafurahia maagizo yako, wala sitalipuuza neno lako.
Na da Dia sema hamoi amoma bagadewane nodonana, amola Dia hamoma: ne sia: i, amo na hamedafa gogolemu.
17 Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi; nitalitii neno lako.
Na da Dia hawa: hamosu dunu. Nama nodone ba: ma. Amasea na da esalawane Dia hamoma: ne olelei amo hamonanumu.
18 Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
Na si Dia fadegalesima, amasea na da Dia sema hamoi moloidafa amo ba: mu.
19 Mimi ni mgeni duniani, usinifiche amri zako.
Na da eso bagahame fawane osobo bagadega esalumu. Amaiba: le, Dia hamoma: ne sia: i amo nama mae wamolegema.
20 Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa juu ya sheria zako wakati wote.
Na da eso huluane Dia moloidafa fofada: su hou dawa: ma: ne bagadewane hanaiba: le, na dogo ganodini se naba.
21 Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.
Di da hidale gasa fibi dunuma gagabole sia: sa. Nowa da Dia hamoma: ne sia: i hame nabasea, gagabusu da ilima aligisa.
22 Niondolee dharau na dhihaka, kwa kuwa ninazishika sheria zako.
Na da ilia gadesu amola higasu hou bu mae ba: ma: ne, Dia na fidima. Bai na da Dia sema huluane nabawane hamonanu.
23 Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia, mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.
Ouligisu dunu da gilisili, na wadela: ma: ne ilegelala. Be na da Dia olelesu amo dawa: digima: ne bai hogosa.
24 Sheria zako ni furaha yangu, nazo ni washauri wangu.
Na da Dia hamoma: ne sia: i hahawane ba: sa. Dia hamoma: ne sia: i liligi huluane da nama fada: i sia: su dunu agoane gala.
25 Nimelazwa chini mavumbini, yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
Na da hasalasiba: le, gulu dabolei diala. Na da Dia ilegele sia: i defele, Dia na esaloma: ne bu uhinisima.
26 Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.
Na da na wadela: i hou hamoi huluane sisane fofada: i. Amola Di da amo nabawane bu dabe adole i. Dia moloidafa hou nama olelema.
27 Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako.
Dia sema hamoi na noga: le dawa: digima: ne, na fidima. Amola na da Dia noga: idafa olelebe noga: le dadawa: lalumu.
28 Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako.
Na da bagadedafa fofagiba: le, hasalasi dagoi ba: sa. Dia ilegei sia: i defele, nama gasa ima.
29 Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako.
Na giadofale ahoasa: besa: le, noga: le ouligima. Dia fidimusa: ilegele sia: i defele, nama gasa ima.
30 Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako.
Na da Dia hou noga: le nabawane hamomusa: ilegei. Na da Dia moloidafa fofada: su noga: le nabawane dadawa: i galu.
31 Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana, usiniache niaibishwe.
Hina Gode! Na da Dia hamoma: ne sia: i, amoma noga: le fa: no bobogei. Na gogosiama: ne mae hamoma.
32 Nakimbilia katika njia ya maagizo yako, kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.
Na da Dia hamoma: ne sia: ne iasu hanaiwane nabawane hamomu. Bai Di da nama fada: ne dawa: su bagade imunu.
33 Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika mpaka mwisho.
Hina Gode! Dia sema ea bai dawa: loma: ne nama olelema. Amola na da Dia sema amoga eso huluane fa: no bobogemu.
34 Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote.
Dia sema ea bai nama noga: le olelema. Amasea, na da na gasa huluane amoga Dia hamoma: ne sia: i fa: no bobogelalumu.
35 Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha.
Dia hamoma: ne sia: i na noga: le fa: no bobogelaloma: ne, Dia ouligima. Bai amo hamoma: ne sia: i da nama hahawane hou iaha.
36 Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.
Di da nama bagade gagumusa: hanasu mae iawane, Dia sema amoma fa: no bobogema: ne hanai fawane nama ima.
37 Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
Na da hamedei liligi amoma bagadewane dawa: sa: besa: le, na amo mae hamoma: ne fidima. Dia ilegele sia: i defele, nama noga: idafa hou hamoma.
38 Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa.
Di da nowa dunu da Dia sia: nabawane hamosea, ema hahawane hamomusa: ilegele sia: i. Amo na da Dia hawa: hamosu dunuba: le, Dia ilegele sia: i amo nama hamoma.
39 Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema.
Na da nama ha lai dunu ilia nama gadesu, amoga beda: sa. Dia na gaga: ma. Dia moloidafa fofada: su hou da noga: idafa.
40 Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako.
Na da Dia hamoma: ne sia: i amo nabawane hamomu hanai gala. Esalusu gaheabolo nama ima. Bai Di da moloidafaba: le.
41 Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
Hina Gode! Dia nama asigi hou da habowaliyale amo nama olelema! Dia ilegele sia: i defele, na gaga: ma!
42 ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.
Amasea, na da dunu amo da nama gadebe, ilima dabe sia: musa: dawa: mu. Bai na Dia sia: dafawaneyale dawa: sa.
43 Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.
Na da eso huluane moloidafa sia: amo sia: noma: ne, Di hamoma. Bai na dafawane hamoma: beyale dawa: su da Dia fofada: su hou amo ganodini diala.
44 Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.
Na da Dia sema huluane, mae fisili, eso huluane nabawane hahamona ahoanumu.
45 Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
Na da halegale noga: ledafa lalalumu. Bai na da Dia olelesu adoba: le fa: no bobogele ba: sa.
46 Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa,
Na da Dia hamoma: ne sia: be, amo hina bagade ilia odagiaba olelemu. Na da hame gogosiamu.
47 kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda.
Na da Dia hamoma: ne sia: i nabawane hamonanebeba: le, hahawane ba: sa. Bai na da amo bagade hanasa.
48 Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.
Na da Dia hamoma: ne sia: i amo gaguia gadosa, amola amoma hanasa. Na da Dia: hamoma: ne sia: i amo dadawa: lalumu.
49 Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako, kwa sababu umenipa tumaini.
Na da Dia hawa: hamosu dunu, amola Di da nama hahawane ilegele sia: beba: le, na da dafawane hamoma: beyale dawa: lusu lai dagoi. Amo ilegele sia: i bu dawa: ma.
50 Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.
Na se nabasu ganodini amolawane, na dogo da denesi. Bai Dia ilegele sia: i da nama fifi ahoanusu i dagoi.
51 Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka, hata hivyo sitaiacha sheria yako.
Hidale gasa fi dunu da eso huluane nama higale ba: sa. Be na Dia sema amo fa: no bobogebe hame yolesi.
52 Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.
Dia musa: hemonega fofada: su hou, na da dawa: lala. Hina Gode! Amo da na dogo denesisa.
53 Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.
Wadela: idafa dunu da Dia sema wadela: lesilalebe na ba: sea, na da ougi bagadewane ba: sa.
54 Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi.
Na da osobo bagadega ode bagahame esalu. Be na da Dia sema olelema: ne, gesami hea: su hahamosa.
55 Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, nami nitatii sheria yako.
Hina Gode! Na da gasia Di fofagini dadawa: lala. Amola na da Dia sema dadawa: lala.
56 Hili limekuwa zoezi langu: nami ninayatii mausia yako.
Na da Dia hamoma: ne sia: i nabawane hamobeba: le, hahawane bagade ba: sa.
57 Ee Bwana, wewe ni fungu langu, nimeahidi kuyatii maneno yako.
Hina Gode! Na da Dima fawane hanai. Na da Dia sema fa: no bobogemusa: ilegele sia: sa.
58 Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote, nihurumie sawasawa na ahadi yako.
Na Dima ha: giwane edegesa! Dia ilegele sia: i defele, na wadela: i hou gogolema: ne olofole, nama asigima.
59 Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
Na da nina: hou abodele, Dia hamoma: ne sia: i amoma fa: no bobogemusa: , ilegele sia: sa.
60 Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.
Mae oualigili, na da hedolowane Dia hamoma: ne sia: i nabawane hamomusa: ahoa.
61 Hata waovu wanifunge kwa kamba, sitasahau sheria yako.
Wadela: i hamosu dunu da na sa: ima: ne sanenesi. Be na da Dia sema hame gogolesa.
62 Usiku wa manane ninaamka kukushukuru kwa sababu ya sheria zako za haki.
Gasi dogoa, na da nedigili, Dia moloidafa fofada: su hou amoma nodosa.
63 Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao, kwa wote wanaofuata mausia yako.
Na da dunu huluane ilia da Dima hawa: hamosa amola Dia sema nabawane hamosa, ili huluane na dogolegei na: iyado agoane ba: sa.
64 Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako, nifundishe maagizo yako.
Hina Gode! Osobo bagade da Dia mae fisili asigidafa hou amoga nabai gala. Dia hamoma: ne sia: i, amo nama olelema.
65 Mtendee wema mtumishi wako Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
Hina Gode! Di da Dia ilegele sia: i didili hamoi dagoi. Na da Dia hawa: hamosu dunu, amola Di da nama noga: le hamosa.
66 Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri, kwa kuwa ninaamini amri zako.
Nama bagade dawa: su amola hamoma: ne dawa: su ima. Bai na da Dia hamoma: ne sia: i amo dafawaneyale dawa: sa.
67 Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.
Musa: , Di da nama se bidi hame i amogalu, na da giadofale ahoasu. Be wali, na da Dia sia: amo nabawane hamosa.
68 Wewe ni mwema, unalotenda ni jema, nifundishe maagizo yako.
Di da noga: idafa amola asigidafa. Dia hamoma: ne sia: i, amo nama olelema.
69 Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo, nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.
Hidale gasa fi dunu da na hou ogogole olelei. Be na da na dogo huluane amoga Dia hamoma: ne sia: i amo nabawane hamonana.
70 Mioyo yao ni katili na migumu, bali mimi napendezwa na sheria yako.
Ilia da asigi dawa: su hame gala. Be na da Dia sema hamonanebeba: le, hahawane ba: sa.
71 Ilikuwa vyema mimi kupata shida ili nipate kujifunza maagizo yako.
Nama se bidi iasu da na hou noga: le fidi. Bai amoga na da Dia hamoma: ne sia: i noga: le dadawa: ahoasu.
72 Sheria inayotoka kinywani mwako ina thamani kubwa kwangu kuliko maelfu ya vipande vya fedha na dhahabu.
Na ba: loba, sema amo Dia nama i, da osobo bagade su huluanedafa baligisa.
73 Mikono yako ilinifanya na kuniumba, nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.
Hina Gode! Di da na hahamoi, amola Di da na gaga: lala. Na da Dia sema huluane dadawa: musa: asigi dawa: su noga: i nama ima.
74 Wakuchao wafurahie wanaponiona, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.
Nowa dunu da Dima nodone dawa: sea, ilia da na ba: sea, nodomu. Bai na da Dia ilegele sia: su amo dafawaneyale dawa: sa.
75 Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki, katika uaminifu wako umeniadhibu.
Hina Gode! Dia fofada: su hou da moloidafa, amo na dawa: Amola dia nama se bidi iasu, bai da Dia mae fisili asigidafa hou olelesa.
76 Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu, sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
Dia mae fisili asigidafa hou da na dogo denesimu da defea. Bai na da Dia hawa: hamosu dunu, amola Di da amo nama defele hamoma: ne sia: i.
77 Huruma yako na inijie ili nipate kuishi, kwa kuwa naifurahia sheria yako.
Na esaloma: ne, Dia nama asigima! Bai na da Dia sema hahawane hamonana.
78 Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu, lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.
Hidale gasa fibi dunu da ogogole nama diwaneya udidiba: le, ilia gogosiamu da defea. Be na da Dia hamoma: ne sia: su amo na asigi dawa: su ganodini dadawa: lalumu.
79 Wale wakuchao na wanigeukie mimi, hao ambao wanazielewa sheria zako.
Nowa dunu da Dima nodosa amola Dia hamoma: ne sia: i noga: le dawa: sa, ilia da nama misunu da defea.
80 Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako, ili nisiaibishwe.
Na da Dia hamoma: ne sia: i noga: ledafa nabawane hamomu da defea. Amasea, na da hame hasalasiba: le, hame gogosiamu.
81 Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako, lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako.
Na da Dia gaga: su hou ba: musa: ouesalebeba: le, na da gufia: i dagoi. Na da Dia sia: fawane dafawaneyale dawa: sa.
82 Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako; ninasema, “Utanifajiri lini?”
Na da Dia ilegele sia: i hou doaga: ma: ne sosodo aligibiba: le, na da si sebe. Na da amane adole ba: sa, “Di da habogala na fidima: bela: ?”
83 Ingawa nimekuwa kama kiriba kwenye moshi, bado sijasahau maagizo yako.
Na da ohe gadofoga waini hano disu ha: digi dagoi defele ba: sa. Be na da Dia hamoma: ne sia: i hame gogolei.
84 Mtumishi wako itampasa angoje mpaka lini? Ni lini utawaadhibu washtaki wangu?
Na da habowali seda ouesaloma: bela: ? Dia da habogala nama se iabe dunu, ilima se dabe ima: bela: ?
85 Wenye majivuno wananichimbia mashimo, kinyume na sheria yako.
Hidale gasa fibi dunu amo da Dia sema nabawane hame hamosa, ilia da na sa: ima: ne uli dogonesi.
86 Amri zako zote ni za kuaminika; unisaidie, kwa sababu watu wananishtaki bila sababu.
Dia hamoma: ne sia: i huluane da dafawaneyale dawa: mu defele gala. Dunu eno ilia da na hou ogogole sia: beba: le, nama se bagade iaha. Dia na fidima!
87 Walikaribia kabisa kunifuta kutoka uso wa dunia, lakini sijaacha mausia yako.
Ilia da na gadenenewane fane legei dagoi. Be na da Dia hamoma: ne sia: su amo hame fisiagai.
88 Yahifadhi maisha yangu sawasawa na upendo wako, nami nitatii sheria za kinywa chako.
Di da eso huluane mae fisili asigidafa hou hamonana. Amaiba: le, Dia nama asigidafa hou hamoma. Amasea, na da Dia sema nabawane hamomu.
89 Ee Bwana, neno lako ni la milele, linasimama imara mbinguni.
Hina Gode! Dia Sia: da eso huluane dialumu. Dia Sia: da Hebene ganodini, eso huluane dialumu.
90 Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote, umeiumba dunia, nayo inadumu.
Dia mae fisili, asigidafa hou da eso huluane dialumu. Di da osobo bagade ea dialoba amogai ligisi. E da amogaiwane diala.
91 Sheria zako zinadumu hadi leo, kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.
Di da liligi huluane ouligisa. Di da amo hamoma: ne sia: beba: le, liligi huluanedafa da ilia dialoba amogaiwane diala.
92 Kama nisingefurahia sheria yako, ningeangamia katika taabu zangu.
Na da se nabawane esalu. Be Dia sema da nama hahawane hou ea bai hame ganiaba, na da se nabawane bogola: loba.
93 Sitasahau mausia yako kamwe, kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
Na da Dia hamoma: ne sia: su amo mae fisili noga: ledafa ouligimu. Bai amoga Di da na esaloma: ne fidi.
94 Uniokoe, kwa maana mimi ni wako, kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
Na da Dia: ! Na fidima! Na da Dia hamoma: ne sia: i amo adoba: le fa: no bobogei.
95 Waovu wanangojea kuniangamiza, bali mimi ninatafakari sheria zako.
Wadela: i hamosu dunu da na fane legema: ne ouesala. Be na da Dia sema amo na asigi dawa: su ganodini dawa: lalumu.
96 Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.
Na da ba: loba, liligi huluane da dagomu bidi gala. Be Dia hamoma: ne sia: i da noga: idafa.
97 Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu. Ninaitafakari mchana kutwa.
Na da Dia sema amoma bagadewane asigisa. Na da hahabe asili daeya, eso huluane amoga Dia sema dadawa: lala.
98 Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu, kwa kuwa nimezishika daima.
Dia hamoma: ne sia: i da eso huluane nama gilisisa. Dia hamoma: ne sia: i da na dawa: su hou amo nama ha lai dunu ilia dawa: su hou baligima: ne hamosa.
99 Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.
Na dawa: su da nama olelesu dunu ilia dawa: su amo baligisa. Bai na da Dia hamoma: ne sia: su amo na asigi dawa: su ganodini dadawa: lala.
100 Nina ufahamu zaidi kuliko wazee, kwa kuwa ninayatii mausia yako.
Na asigi dawa: su da da: i hamoi dunu ilia asigi dawa: su baligisa. Bai na da Dia hamoma: ne sia: su amo nabawane hamosa.
101 Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya, ili niweze kutii neno lako.
Na da wadela: i hou hamosu amoma hame gilisi. Bai na da Dia sia: nabawane hamomusa: hanai gala.
102 Sijaziacha sheria zako, kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.
Na da Dia hamoma: ne sia: su hame fisiagasu. Bai Dia Disu da na Olelesu Dunu.
103 Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu, matamu kuliko asali katika kinywa changu!
Dia hamoma: ne sia: su da hedai bagade. Ilia hedai da agime hano ea hedai baligisa.
104 Ninapata ufahamu kutoka mausia yako, kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.
Dia sema da bagade dawa: su nama iaha. Amaiba: le, na da wadela: i hou hamobe huluane higasa.
105 Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga katika njia yangu.
Dia sia: da nama logo olelesu gamali defele gala. Dia sia: da na logo ba: ma: ne hadigi digagala: sa
106 Nimeapa na nimethibitisha, kwamba nitafuata sheria zako za haki.
Na da Dia moloidafa hamoma: ne sia: i amo nabawane hamomusa: ilegele sia: i dagoi. Amo ilegele sia: i, na da hame gogolemu.
107 Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
Hina Gode! Na da baligiliwane se naba. Dia musa: ilegele sia: i defele, na mae bogole esaloma: ne fidima.
108 Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu, nifundishe sheria zako.
Hina Gode! Na Dima nodone sia: ne gadosu amo nabima. Dia hamoma: ne sia: su amo nama olelema.
109 Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote, sitasahau sheria yako.
Na Dima fa: no bobogemusa: , na esalusu fisimusa: momagele esala. Na da Dia sema hame gogolei.
110 Waovu wamenitegea mtego, lakini sijayakiuka maagizo yako.
Wadela: i hamosu dunu da na sa: ima: ne sanenesisa. Be na da Dia hamoma: ne sia: i mae fisili nabawane hamonana.
111 Sheria zako ni urithi wangu milele, naam ni furaha ya moyo wangu.
Na da Dia hamoma: ne sia: su mae fisili, eso huluane gagui dialebe ba: mu. Dia hamoma: ne sia: i da nama hahawane hou iaha.
112 Nimekusudia moyoni mwangu kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.
Na da agoane ilegei dagoi. Na da Dia sema amo fa: no bobogelaleawane, na bogomu eso doaga: mu.
113 Ninachukia watu wa nia mbili, lakini ninapenda sheria yako.
Dunu amo da Dima noga: le hame fa: no bobogebe, na da higasa. Be na da Dia sema amoma asigisa.
114 Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu, nimeweka tumaini langu katika neno lako.
Di da na gesu amola na gaga: su. Na dafawane hamoma: beyale dawa: su ea bai da Dia ilegele sia: su.
115 Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
Dili wadela: i hamosu dunu! Gasigama! Na da na Gode Ea hamoma: ne sia: i nabawane hamomu.
116 Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
Hina Gode! Dia ilegele sia: i defele, nama gasa ima! Amasea, na da esalumu. Na dafawane hamoma: beyale dawa: su fisisa: besa: le, Dia fidima.
117 Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.
Na dafasa: besa: le, na gaguma. Amasea, na da gaga: i dagoi ba: mu. Amola na da mae fisili, Dia hamoma: ne sia: i dadawa: lalu, nabawane hamomu.
118 Unawakataa wote wanaoyaasi maagizo yako, kwa maana udanganyifu wao ni bure.
Di da nowa dunu da Dia sema nabawane hame hamosea, Di da ili higale fisiagasa. Ilia ogogole ilegesu da hamedei liligi.
119 Waovu wa nchi unawatupa kama takataka, kwa hivyo nazipenda sheria zako.
Di da wadela: i hamosu dunu huluane isu agoane ha: digisa. Amaiba: le, na da Dia hamoma: ne sia: i amoma nodosa.
120 Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe, ninaziogopa sheria zako.
Na da Diba: le beda: sa. Dia moloidafa fofada: su houba: le, na da bagadewane beda: sa.
121 Nimetenda yaliyo haki na sawa, usiniache mikononi mwa watesi wangu.
Na da hou noga: idafa amola moloidafa hamoi dagoi. Na ha lai dunu da na hasalasisa: besa: le, na mae yolesima.
122 Mhakikishie mtumishi wako usalama, usiache wenye kiburi wanionee.
Na da Dia hawa: hamosu dunuba: le, Dia na fidima: ne ilegele sia: ma. Hidale gasa fifi dunu da na banenesisa: besa: le, Dia na fidima.
123 Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako, na kuitazamia ahadi yako ya kweli.
Na da Dia gaga: musa: ilegele sia: i amo nama doaga: ma: ne, sosodo ouesalebeba: le, na da si sebe.
124 Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako na unifundishe maagizo yako.
Dia mae fisili asigidafa hou defele, Dia na fidima. Amola Dia hamoma: ne sia: su nama olelema.
125 Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu ili niweze kuelewa sheria zako.
Na da Dia hawa: hamosu dunu. Na da Dia olelesu noga: le dawa: musa: , asigi dawa: su bagade nama ima.
126 Ee Bwana, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.
Hina Gode! Dia hawa: hamomu eso da doaga: i dagoi. Bai dunu ilia da Dia sema nabawane hame hamosa.
127 Kwa sababu nazipenda amri zako zaidi ya dhahabu, naam, zaidi ya dhahabu safi,
Na da Dia hamoma: ne sia: su amoma hanai hou da gouli noga: idafa amoma hanai hou bagadewane baligisa.
128 na kwa sababu naona maagizo yako yote ni adili, nachukia kila njia potovu.
Amaiba: le, na da Dia hamoma: ne sia: su huluane amoma fa: no bobogesa. Na da wadela: i hamosu logo amoga masunu higasa.
129 Sheria zako ni za ajabu, hivyo ninazitii.
Dia olelesu da noga: idafa. Na da na dogoa asigi dawa: su huluane amoga Dia olelesu nabawane hamosa.
130 Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru, kunampa mjinga ufahamu.
Dunu ilia da Dia olelesu liligi amo dawa: loma: ne olelesea, hadigi da maha amola hame dawa: su dunu da asigi dawa: su laha.
131 Nimefungua kinywa changu na kuhema, nikitamani amri zako.
Na da Dia hamoma: ne sia: su dawa: musa: bagadewane hanaiba: le, na da helega ha: ha: sa.
132 Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote wale wanaolipenda jina lako.
Dia da Dima asigi dunu huluane ilima hamobe defele, nama ba: leguda: le, asigima.
133 Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako, usiache dhambi yoyote initawale.
Dia ilegele sia: i defele, na dafasa: besa: le, amola wadela: i houga hasalasisa: besa: le, na fidima.
134 Niokoe na uonevu wa wanadamu, ili niweze kutii mausia yako.
Na da Dia hamoma: ne sia: i noga: le nabawane hamomusa: , nama ha lai dunu da na mae banenesima: ne, Dia na gaga: ma.
135 Mwangazie mtumishi wako uso wako na unifundishe amri zako.
Na hahawane ganoma: ne, Di nama misini, amola Dia sema nama olelema.
136 Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu, kwa kuwa sheria yako haifuatwi.
Na si hano da hano yogo agoane daha. Bai dunu eno ilia Dia sema nabawane hame hamosa.
137 Ee Bwana, wewe ni mwenye haki, sheria zako ni sahihi.
Hina Gode! Di da moloidafa, amola Dia sema da moloidafa fofada: musa: defele gala.
138 Sheria ulizoziweka ni za haki, ni za kuaminika kikamilifu.
Hamoma: ne sia: i Dia i da dafawane moloidafa amola moloidafa fofada: musa: defele gala.
139 Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu wanayapuuza maneno yako.
Na ougi hou da na dogo ganodini lalu agoane nenana. Bai na ha lai dunu ilia da Dia hamoma: ne sia: su da hamedei liligi agoai ba: sa.
140 Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu, mtumishi wako anazipenda.
Dia ilegele sia: i da dafawanedafa dialumu. Na da Dia ilegele sia: i bagadewane hanasa.
141 Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa, sisahau mausia yako.
Na da hamedei dunu agoai, amola eno dunu ilia da na higasa. Be na da Dia olelesu liligi hame fisiagasa.
142 Haki yako ni ya milele, na sheria yako ni kweli.
Dia moloidafa hou da mae fisili eso huluane dialumu. Dia sema da eso huluane dafawanedafa diala.
143 Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.
Na da da: i dioi bagade amola bidi hamosu bagade ba: sa. Be Dia hamoma: ne sia: su da nama hahawane hou iaha.
144 Sheria zako ni sahihi milele, hunipa ufahamu ili nipate kuishi.
Dia hamoma: ne sia: su da eso huluane moloidafa fofada: su defele gala. Na esaloma: ne, asigi dawa: su noga: i amo nama ima.
145 Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
Na asigi dawa: su huluane amoga na dima wele sia: sa. Hina Gode! Na sia: be amo dabe adole ima. Amasea, na da Dia hamoma: ne sia: su amo nabawane hamomu.
146 Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
Na Dima wele sia: sa. Na gaga: ma! Amasea, na da Dia sema didili hamomu.
147 Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
Eso da hame misia, na da Dia na fidima: ne wele sia: sa. Na da Dia ilegele sia: i nababeba: le, na da dafawane hamoma: beyale dawa: lusu lai dagoi.
148 Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
Daeya ganini hadigibi galu, na da mae golale si dagane esala, Dia hamoma: ne sia: su dadawa: sa esala.
149 Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
Hina Gode! Dia asigidafa hou da mae fisili dialebeba: le, na sia: nabima. Na esaloma: ne, Dia gogolema: ne olofole asigidafa hou nama olelema.
150 Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako.
Nama se iabe dunu da dodona: gi, amola Dia sema hamedafa fa: no bobogesa. Ilia nama gadenena maha.
151 Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli.
Be Hina Gode! Di da na gadenene lela, amola Dia hamoma: ne sia: su da eso huluane dialumu.
152 Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
Musa: ganiniwane, na da Dia hamoma: ne sia: i amoga dawa: lai. Dia hamoma: ne sia: i da eso huluane dialoma: ne hahamoi.
153 Yaangalie mateso yangu, uniokoe, kwa kuwa sijasahau sheria yako.
Na se nabasu ba: ma! Amola na gaga: ma! Bai na da Dia sema noga: le ouligi.
154 Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.
Na hamobe hou amo gaga: ma, amola na halegale esaloma: ne hamoma. Dia ilegele sia: i defele, na gaga: ma.
155 Wokovu uko mbali na waovu, kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.
Wadela: i hamosu dunu da gaga: su hame ba: mu. Bai ilia da Dia sema nabawane hame hamosa.
156 Ee Bwana, huruma zako ni kuu, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.
Be Hina Gode! Di hahanibi dunuma bagadedafa asigisa. Dia gogolema: ne olofole asigi hou nama olelema, amola na gaga: ma.
157 Adui wanaonitesa ni wengi, lakini mimi sitaziacha sheria zako.
Nama ha lai dunu amola nama banenesisu dunu da bagohame esafula. Be na da Dia sema fa: no bobogesu hame fisisa.
158 Ninawatazama wasioamini kwa chuki, kwa kuwa hawalitii neno lako.
Na da amo hohonosu dunu ba: sea, na da bagadewane higale ba: sa. Bai ilia da Dia hamoma: ne sia: i amoma hame fa: no bobogesa.
159 Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako; Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.
Hina Gode! Ba: ma! Na da Dia hamoma: ne sia: su bagadewane hanasa. Dia asigidafa hou da afadenesu hame dawa: Amaiba: le, na gaga: ma!
160 Maneno yako yote ni kweli, sheria zako zote za haki ni za milele.
Dia sema bai da dafawanedafa hou. Amola Dia moloidafa fofada: su huluane da eso huluane dialumu.
161 Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
Gasa bagade dunu da bai hamedene, udigili nama doagala: sa. Be na da Dia sema amo fa: no bobogesa.
162 Nafurahia ahadi zako kama mtu aliyepata mateka mengi.
Dunu amo da gobolo liligi bagadedafa hahawane hogole ba: sea, amo defele na da Dia ilegele sia: su ba: sea, hahawane bagade gala.
163 Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo, lakini napenda sheria yako.
Na da ogogosu hou huluane bagade higasa. Be na da Dia sema bagade hanasa.
164 Ninakusifu mara saba kwa siku, kwa ajili ya sheria zako za haki.
Di da moloidafa fofada: su hou hamonanebeba: le, na da eso huluane amoga, fesuale agoane Dima nodone sia: sa.
165 Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
Nowa da Dia sema hamoma: ne hanaiwane esalea, ilia da gaga: iwane esala. Ilia da dafasu hame dawa:
166 Ee Bwana, ninangojea wokovu wako, nami ninafuata amri zako,
Hina Gode! Dia na gaga: ma: ne, na da ouesala. Amola na da Dia hamoma: ne sia: be defele hamonana.
167 Ninazitii sheria zako, kwa sababu ninazipenda mno.
Na da Dia olelesu nabawane hamonana. Na da na dogo huluane amoga Dia olelesu hanasa.
168 Nimetii mausia yako na sheria zako, kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.
Na da Dia hamoma: ne sia: su amo nabawane hamosa. Dia da na hamobe huluane ba: lala.
169 Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako, nipe ufahamu sawasawa na neno lako.
Hina Gode! Na fidima: ne digini wele sia: su amo Dima doaga: ma: ne, logo doasima. Dia ilegele sia: i defele, dawa: lama: ne asigi dawa: su nama ima.
170 Maombi yangu na yafike mbele zako, niokoe sawasawa na ahadi yako.
Na sia: ne gadobe nabima. Amola Dia hamomusa: ilegei defele, na gaga: ma!
171 Midomo yangu na ibubujike sifa, kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.
Na da eso huluane Dima nodone sia: nanumu. Bai Di da nama, Dia sema amo olelesa.
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, kwa kuwa amri zako zote ni za haki.
Na da Dia sema amoga gesami lale hea: mu. Bai Dia hamoma: ne sia: su da moloi fofada: musa: defele gala.
173 Mkono wako uwe tayari kunisaidia, kwa kuwa nimechagua mausia yako.
Di eso huluane, na fidimusa: , momagele ouesaloma. Bai na da Dia hamoma: ne sia: su amoma fa: no bobogelala.
174 Ee Bwana, ninatamani wokovu wako, na sheria yako ni furaha yangu.
Hina Gode! Dia fidima: ne gaga: su hou nama doaga: ma: ne, na da bagadewane hanasa. Na da Dia sema amo ganodini hahawane hou ba: sa.
175 Nijalie kuishi ili nipate kukusifu, na sheria zako zinitegemeze.
Na da Dima nodone sia: nanumusa: , esalusu nama ima. Dia hamoma: ne sia: su na fidimu da defea.
176 Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea. Mtafute mtumishi wako, kwa kuwa sijasahau amri zako.
Na da sibi fisi defele, doulalala. Na da Dia hawa: hamosu dunu. Amaiba: le, Dia na hogomusa: misa! Bai na da Dia hamoma: ne sia: i noga: le ouligi.

< Zaburi 119 >