< Zaburi 118 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Aleluja! Zahvaljujte Jahvi jer je dobar, jer je vječna ljubav njegova!
2 Israeli na aseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
Neka rekne dom Izraelov: “Vječna je ljubav njegova!”
3 Nyumba ya Aroni na iseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
Neka rekne dom Aronov: “Vječna je ljubav njegova!”
4 Wote wamchao Bwana na waseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
Svi koji se Jahve boje neka reknu: “Vječna je ljubav njegova!”
5 Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.
Iz tjeskobe Jahvu ja zazvah: on me usliša i oslobodi.
6 Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
Jahve je sa mnom i ja ne strahujem: što mi tko može?
7 Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
Jahve je sa mnom, pomoć moja, i zbunjene gledam dušmane.
8 Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
Bolje se Jahvi uteći nego se uzdat' u čovjeka.
9 Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
Bolje se Jahvi uteći nego se uzdat' u mogućnike.
10 Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Pogani me okružiše: imenom ih Jahvinim uništih.
11 Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Opkoliše me odasvud: imenom ih Jahvinim uništih.
12 Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Opkoliše me poput pčela, ubod im žeže kao trnje zapaljeno: imenom ih Jahvinim uništih.
13 Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
Gurahu me, gurahu, da me obore, ali mi Jahve pomože.
14 Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
Jahve je moja snaga i pjesma, on mi je spasitelj.
15 Sauti za shangwe na ushindi zinavuma hemani mwa wenye haki: “Mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!
Čuj! Radost i spasenje odzvanja šatorima pravednika: Jahvina se proslavi desnica,
16 Mkono wa kuume wa Bwana umeinuliwa juu, mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!”
Jahvina me uzdigne desnica, Jahvina se proslavi desnica!
17 Sitakufa, bali nitaishi, nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
Ne, umrijeti neću nego živjeti i kazivat ću djela Jahvina.
18 Bwana ameniadhibu vikali, lakini hakuniacha nife.
Kaznom teškom kaznio me Jahve, ali me smrti ne preda.
19 Nifungulie malango ya haki, nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
Otvorite mi širom vrata pravde: ući ću, Jahvi zahvalit'!
20 Hili ni lango la Bwana ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
“Ovo su vrata Jahvina, na njih ulaze pravedni!”
21 Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, umekuwa wokovu wangu.
Zahvalit ću ti što si me uslišio i moj postao spasitelj.
22 Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Kamen što ga odbaciše graditelji postade kamen zaglavni.
23 Bwana ametenda hili, nalo ni la kushangaza machoni petu.
Jahvino je to djelo: kakvo čudo u očima našim!
24 Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, tushangilie na kufurahi ndani yake.
Ovo je dan što ga učini Jahve: kličimo i radujmo se njemu!
25 Ee Bwana, tuokoe, Ee Bwana, utujalie mafanikio.
O Jahve, spasenje nam daj! Jahve, sreću nam daj!
26 Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
Blagoslovljen koji dolazi u imenu Jahvinu! Blagoslivljamo vas iz Doma Jahvina!
27 Bwana ndiye Mungu, naye ametuangazia nuru yake. Mkiwa na matawi mkononi, unganeni kwenye maandamano ya sikukuu hadi kwenye pembe za madhabahu.
Obasjao nas Bog Jahve! Složite povorku s grančicama u ruci sve do rogova žrtvenika.
28 Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
Ti si Bog moj - tebi zahvaljujem: Bože moj, tebe ja uzvisujem.
29 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Zahvaljujte Jahvi jer je dobar, jer je vječna ljubav njegova!

< Zaburi 118 >