< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Det är mig ljuft, att Herren hörer mina röst och mina bön;
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Att han böjer sina öron till mig; derföre vill jag åkalla honom i mina lifsdagar.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Dödsens snaror hade omfattat mig, och helvetes ångest hade råkat uppå mig; jag kom i jämmer och nöd. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Men jag åkallade Herrans Namn: O! Herre, fräls mina själ.
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Herren är nådelig och rättfärdig, och vår Gud är barmhertig.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Herren bevarar de enfaldiga; när jag nederligger så hjelper han mig.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Var nu åter tillfrids, min själ; ty Herren gör dig godt.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Ty du hafver uttagit mina själ utu dödenom, mina ögon ifrå tårar, min fot ifrå fall.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Jag vill vandra för Herranom uti de lefvandes lande.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Jag tror, derföre talar jag; men jag varder svårliga plågad.
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Jag sade i min häpenhet: Alla menniskor äro lögnaktige.
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
Huru skall jag vedergälla Herranom alla hans välgerningar, som han mig gör?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Jag vill taga den helsosamma kalken, och predika Herrans Namn.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Jag vill betala mina löften Herranom, för allt folk.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Hans helgons död är dyr hållen för Herranom.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
O! Herre, jag är din tjenare; jag är din tjenare, dine tjenarinnos son; du hafver sönderslitit mina band.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Dig vill jag offra tacksägelse, och predika Herrans Namn.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
Jag vill betala mina löften Herranom, för allt hans folk;
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Uti gårdarna åt Herrans hus, uti dig, Jerusalem. Halleluja.

< Zaburi 116 >