< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Amo al SEÑOR, porque ha oído mi voz y mis súplicas.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Porque ha inclinado a mí su oído, le invocaré en todos mis días.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Me rodearon los dolores de la muerte, me encontraron las angustias del sepulcro; angustia y dolor había yo hallado. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Entonces invoqué el Nombre del SEÑOR, diciendo: Libra ahora, oh SEÑOR, mi alma.
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Clemente es el SEÑOR y justo; sí, misericordioso es nuestro Dios.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
El SEÑOR guarda a los simples; estaba debilitado, y me salvó.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Vuelve, oh alma mía, a tu reposo; porque el SEÑOR te ha hecho bien.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Porque has librado mi alma de la muerte, mis ojos de lágrimas, y mis pies de resbalar.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Andaré delante del SEÑOR en la tierra de los vivientes.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Creí; por tanto hablé, y fui afligido en gran manera.
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Y dije en mi apresuramiento: Todo hombre es mentiroso.
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
¿Qué pagaré al SEÑOR por todos sus beneficios para conmigo?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Tomaré la copa de la salud, e invocaré el Nombre del SEÑOR.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Ahora pagaré mis votos al SEÑOR delante de todo su pueblo.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Estimada es en los ojos del SEÑOR la muerte de sus misericordiosos.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Así es oh SEÑOR, porque yo soy tu siervo, yo soy tu siervo, hijo de tu sierva; tú rompiste mis prisiones.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Te ofreceré sacrificio de alabanza, e invocaré el Nombre del SEÑOR.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
Ahora pagaré mis votos al SEÑOR delante de todo su pueblo;
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
en los atrios de la Casa del SEÑOR, en medio de ti, oh Jerusalén. Alelu-JAH.

< Zaburi 116 >