< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Yo amo al Señor porque Él me escucha, escucha mi clamor pidiendo ayuda.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Lo invocaré mientras viva porque Él atiende lo que digo.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Estuve atrapado por las trampas de la muerte; Estuve cautivo por los terrores de la tumba. Todo lo que experimenté fue dolor y sufrimiento. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Entonces clamé al Señor, “¡Dios, por favor, sálvame!”
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
¡El Señor es justo y bueno! ¡Nuestro Dios es un Dios compasivo!
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
El Señor cuida de los indefensos; cuando fui derribado Él me salvó.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Puedo estar en paz otra vez porque el Señor ha sido bueno conmigo.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Porque me has salvado de la muerte, has detenido mi llanto, y me has salvado de caer.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Ahora puedo caminar con el Señor en la tierra de los vivos.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Confié en ti, y clamé a ti diciendo, “¡Estoy sufriendo terriblemente!”
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Estaba tan molesto que dije, “¡Todos son unos mentirosos!”
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
¿Qué puedo darle al Señor en agradecimiento por todo lo que ha hecho por mí?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Levantaré la copa de la salvación y adoraré al Señor.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Cumpliré mis promesas al Señor para que todos puedan ver.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Le duele al Señor cuando mueren aquellos que ama.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Señor, realmente soy tu siervo, te sirvo tal y como y mi madre lo hizo antes de mí, sin embargo, tú me has liberado.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Te ofreceré sacrificio en acción de gracias y te alabaré.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
Cumpliré mis promesas en presencia de todo tu pueblo,
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
en la casa del Señor, justo en Jerusalén. ¡Alabado sea el Señor!

< Zaburi 116 >