< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Amo ao Senhor, porque elle ouviu a minha voz e a minha supplica.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Porque inclinou a mim os seus ouvidos; portanto o invocarei emquanto viver.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Os cordeis da morte me cercaram, e angustias do inferno se apoderaram de mim: encontrei aperto e tristeza. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Então invoquei o nome do Senhor, dizendo: Ó Senhor, livra a minha alma.
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Piedoso é o Senhor e justo: o nosso Deus tem misericordia.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
O Senhor guarda aos simplices: fui abatido, mas elle me livrou.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Alma minha, volta para o teu repouso, pois o Senhor te fez bem.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Porque tu, Senhor, livraste a minha alma da morte, os meus olhos das lagrimas, e os meus pés da queda.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Andarei perante a face do Senhor na terra dos viventes.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Cri, por isso fallei: estive muito afflicto.
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Dizia na minha pressa: Todos os homens são mentirosos.
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
Que darei eu ao Senhor, por todos os beneficios que me tem feito?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Tomarei o calix da salvação, e invocarei o nome do Senhor.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Pagarei os meus votos ao Senhor, agora, na presença de todo o seu povo.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Preciosa é á vista do Senhor a morte dos seus sanctos.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Ó Senhor, devéras sou teu servo: sou teu servo, filho da tua serva; soltaste as minhas ataduras.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Offerecer-te-hei sacrificios de louvor, e invocarei o nome do Senhor.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
Pagarei os meus votos ao Senhor, na presença de todo o meu povo.
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Nos atrios da casa do Senhor, no meio de ti, ó Jerusalem. Louvae ao Senhor.

< Zaburi 116 >