< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
IO amo [il Signore]; perciocchè egli ascolta La mia voce, [e] le mie supplicazioni.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Poichè egli ha inchinato a me il suo orecchio, Io [lo] invocherò tutti i giorni della mia vita.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
I legami della morte mi avevano circondato, E le distrette del sepolcro mi avevano colto; Io aveva scontrata angoscia e cordoglio. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Ma io invocai il Nome del Signore, [Dicendo: ] Deh! Signore, libera l'anima mia.
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Il Signore [è] pietoso e giusto; E il nostro Dio è misericordioso.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Il Signore guarda i semplici; Io era ridotto in misero stato, Ed egli mi ha salvato.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Ritorna, anima mia, al tuo riposo; Perciocchè il Signore ti ha fatta la tua retribuzione.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Poichè, [o Signore], tu hai ritratta l'anima mia da morte, Gli occhi miei da lagrime, I miei piedi da caduta;
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Io camminerò nel tuo cospetto Nella terra de' viventi.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Io ho creduto, [e però] certo io parlerò. Io era grandemente afflitto;
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Io diceva nel mio smarrimento: Ogni uomo [è] bugiardo.
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
Che renderò io al Signore? Tutti i suoi beneficii [son] sopra me.
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Io prenderò il calice delle salvazioni, E predicherò il Nome del Signore.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Io pagherò i miei voti al Signore, Ora in presenza di tutto il suo popolo.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
La morte de' santi del Signore [È] preziosa nel suo cospetto.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Deh! Signore, [esaudiscimi]; perciocchè io [son] tuo servitore; Io [son] tuo servitore, figliuolo della tua servente; Tu hai sciolti i miei legami.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Io ti sacrificherò sacrificio di lode, E predicherò il Nome del Signore.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
Io pagherò i miei voti al Signore, Ora in presenza di tutto il suo popolo;
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Ne' cortili della Casa del Signore, In mezzo di te, o Gerusalemme. Alleluia.

< Zaburi 116 >