< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Ina ƙaunar Ubangiji, gama ya ji muryata; ya ji kukata ta neman jinƙai.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Domin ya juye kunnensa gare ni, zan kira gare shi muddin ina da rai.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Igiyoyin mutuwa sun shaƙe ni, wahalar kabari sun zo a kaina; na cika da wahala da ɓacin rai. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Sai na kira ga sunan Ubangiji na ce, “Ya Ubangiji, ka cece ni!”
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Ubangiji mai alheri ne da kuma mai adalci; Allahnmu yana cike da tausayi.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Ubangiji yana tsare masu tawali’u; sa’ad da nake cikin tsananin bukata, ya cece ni.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Ka kwantar da hankali, ya raina, gama Ubangiji mai alheri ne a gare ka.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Gama kai, ya Ubangiji, ka ceci raina daga mutuwa, idanuna daga hawaye, ƙafafuna daga tuntuɓe,
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
don in iya tafiya a gaban Ubangiji a ƙasar masu rai.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Na gaskata, saboda haka na ce, “An azabtar da ni ƙwarai.”
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Kuma cikin rikicewana na ce, “Dukan mutane maƙaryata ne.”
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
Yaya zan sāka wa Ubangiji saboda dukan alherinsa gare ni?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Zan daga kwaf na ceto in kuma kira ga sunan Ubangiji.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Zan cika alkawurana ga Ubangiji a gaban dukan mutanensa.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Abu mai daraja a gaban Ubangiji shi ne mutuwar tsarkakansa.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Ya Ubangiji, da gaske ni bawanka ne; ni bawanka ne, ɗan baiwarka; ka’yantar da ni daga sarƙoƙi.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Zan yi hadayar godiya gare ka in kuma kira bisa sunan Ubangiji.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
Zan cika alkawurana ga Ubangiji a gaban dukan mutanensa,
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
a filayen gidan Ubangiji, a tsakiyarki, ya Urushalima. Yabi Ubangiji.

< Zaburi 116 >