< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Jahwe hab ich lieb, / Denn er hat meine Stimme, mein Flehn erhört.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Ja, er hat mir sein Ohr zugeneigt; / Drum werd ich ihn auch, solang ich lebe, anrufen.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Mich hatten des Todes Bande umringt, / Ich fürchtete schon, ins Grab zu sinken, / Angst und Kummer erfuhr ich. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Da rief ich Jahwes Namen an: / "Ach, Jahwe, rette mein Leben!"
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Jahwe war auch gnädig und treu, / Und es erbarmte sich unser Gott.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Schutzlose behütet Jahwe: / Drum half er mir auch, als ich elend war.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
"Kehr nun ein, meine Seele, in deine Ruh, / Denn Jahwe hat dir wohlgetan!"
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Ja, du hast meine Seele dem Tode entrissen, / Meinen Augen die Tränen getrocknet, / Meinen Fuß vor Gleiten bewahrt.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
So darf ich vor Jahwe noch wandeln / In der Lebendigen Landen.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Ich sprach die Wahrheit, als ich sagte: / "Ich bin sehr niedergedrückt."
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Ich habe sogar in meiner Angst gesagt: / "Alle Menschen sind Lügner."
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
Wie soll ich nun aber Jahwe vergelten / All seine Wohltaten, die ich erfahren?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Den Becher des Heils werd ich erheben / Und Jahwes Namen anrufen.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Meine Gelübde werd ich Jahwe erfüllen / Frei und offen vor all seinem Volk.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Selten nur läßt Jahwe / Seine Frommen (frühzeitig) sterben.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Ach Jahwe, (erhalte darum mein Leben auch ferner)! / Ich bin ja dein Knecht. / Ich bin dein Knecht, der Sohn deiner Magd. / Du hat meine Fesseln gelöst.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Dir will ich Dankopfer bringen / Und Jahwes Namen anrufen.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
Meine Gelübde will ich Jahwe erfüllen / Frei und offen vor all seinem Volk.
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
In den Vorhöfen des Hauses Jahwes, / In der Mitte, Jerusalem! / Lobt Jah!

< Zaburi 116 >