< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Je l'aime, car Yahweh entend ma voix, mes supplications.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Car il a incliné vers moi son oreille, et toute ma vie, je l'invoquerai.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Les liens de la mort m'entouraient, et les angoisses du schéol m'avaient saisi; j'étais en proie à la détresse et à l'affliction. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Et j'ai invoqué le nom de Yahweh: « Yahweh, sauve mon âme! »
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Yahweh est miséricordieux et juste, notre Dieu est compatissant.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Yahweh garde les faibles; j'étais malheureux, et il m'a sauvé.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Mon âme, retourne à ton repos; car Yahweh te comble de biens.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Oui, tu as sauvé mon âme de la mort, mon œil des larmes, mes pieds de la chute.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Je marcherai encore devant Yahweh, dans la terre des vivants.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
J'ai confiance, alors même que je dis: « je suis malheureux à l'excès. »
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Je disais dans mon abattement: « Tout homme est menteur. »
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
Que rendrai-je à Yahweh pour tous ses bienfaits à mon égard!
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
J'élèverai la coupe du salut, et j'invoquerai le nom de Yahweh.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
J'accomplirai mes vœux envers Yahweh en présence de tout son peuple.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Elle a du prix aux yeux de Yahweh, la mort de ses fidèles.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Ah! Yahweh, parce que je suis ton serviteur, ton serviteur, fils de ta servante, tu as détaché mes liens.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Je t'offrirai un sacrifice d'actions de grâces, et j'invoquerai le nom de Yahweh.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
J'accomplirai mes vœux envers Yahweh, en présence de tout son peuple,
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
dans les parvis de la maison de Yahweh, dans ton enceinte, Jérusalem. Alleluia!

< Zaburi 116 >