< Zaburi 116 >
1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Halleluja! Ik heb Jahweh lief, Want Hij hoort naar mijn smeken!
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Hij luisterde naar mij, toen ik riep
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol )
En de strikken des doods mij omknelden; Toen doodsangst mij kwelde, Nood en jammer mij troffen. (Sheol )
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Ik riep de Naam van Jahweh aan: "Ach, Jahweh, spaar toch mijn leven!"
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
En Jahweh was genadig en trouw, Onze God vol ontferming:
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Jahweh waakt over de zwakken; Ik was uitgeput, maar Jahweh heeft mij gered!
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Wees dan gelaten, mijn ziel; Want Jahweh blijft voor u zorgen:
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Hij heeft mij gered van de dood, Mijn ogen van tranen, mijn voeten van stoten;
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Nog mag ik voor Jahweh’s aanschijn wandelen In de landen der levenden!
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Ik blijf dus vertrouwen, al roep ik ook uit: "Ik ben diep ongelukkig!"
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Al zou ik in mijn ellende ook zeggen: "Er is geen mens te vertrouwen!"
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
Hoe zal ik Jahweh kunnen vergelden Al het goede, dat Hij mij deed?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
De kelk der redding hef ik omhoog, En roep de Naam van Jahweh aan;
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
Ik zal mijn gelofte aan Jahweh volbrengen Ten overstaan van heel het volk:
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Want te duur was in de ogen van Jahweh De dood zijner vromen.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Ach Jahweh, ik ben maar uw knecht, de zoon van uw dienstmaagd, Toch hebt Gij mijn boeien verbroken:
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Ik breng U dan een offer van dank, En roep de Naam van Jahweh aan,
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
In de voorhoven van Jahweh’s huis, Binnen uw muren, Jerusalem!