< Zaburi 115 >
1 Sio kwetu sisi, Ee Bwana, sio kwetu sisi, bali utukufu ni kwa jina lako, kwa sababu ya upendo na uaminifu wako.
Niet ons, o Jahweh, niet ons, Maar uw Naam geef eer om uw goedheid en trouw!
2 Kwa nini mataifa waseme, “Yuko wapi Mungu wao?”
Waarom zouden de heidenen zeggen: "Waar is toch hun God?"
3 Mungu wetu yuko mbinguni, naye hufanya lolote limpendezalo.
De God van òns is in de hemel, En Hij doet wat Hij wil;
4 Lakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Doch hùn goden zijn maar zilver en goud, Door mensenhanden gemaakt.
5 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Ze hebben een mond, maar kunnen niet spreken; Ogen, maar kunnen niet zien;
6 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, zina pua, lakini haziwezi kunusa;
Oren, maar kunnen niet horen; Een neus, maar kunnen niet ruiken.
7 zina mikono, lakini haziwezi kupapasa, zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala koo zao haziwezi kutoa sauti.
Hun handen kunnen niet tasten, Hun voeten niet gaan; Ze geven geen geluid met hun keel, En hebben geen adem in hun mond.
8 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Aan hen worden gelijk, die ze maken, En allen, die er op hopen!
9 Ee nyumba ya Israeli, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
Maar Israël blijft op Jahweh vertrouwen: Hij is hun hulp en hun schild;
10 Ee nyumba ya Aroni, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
Het huis van Aäron blijft op Jahweh vertrouwen: Hij is hun hulp en hun schild;
11 Ninyi mnaomcha, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
Die Jahweh vrezen, blijven op Jahweh vertrouwen: Hij is hun hulp en hun schild!
12 Bwana anatukumbuka na atatubariki: ataibariki nyumba ya Israeli, ataibariki nyumba ya Aroni,
En Jahweh zal ons gedenken, Ons zijn zegen verlenen: Het huis van Israël zegenen, Het huis van Aäron zegenen,
13 atawabariki wale wanaomcha Bwana, wadogo kwa wakubwa.
Die Jahweh vrezen zegenen, Kleinen en groten;
14 Bwana na awawezeshe kuongezeka, ninyi na watoto wenu.
En Jahweh zal u blijven zegenen, U en uw kinderen!
15 Mbarikiwe na Bwana Muumba wa mbingu na dunia.
Weest dan gezegend door Jahweh, Die hemel en aarde heeft gemaakt:
16 Mbingu zilizo juu sana ni mali ya Bwana, lakini dunia amempa mwanadamu.
De hemel blijft de hemel van Jahweh, Maar de aarde gaf Hij aan de kinderen der mensen.
17 Sio wafu wanaomsifu Bwana, wale washukao mahali pa kimya,
De doden zullen Jahweh niet prijzen, Niemand, die in het oord van Stilte is gedaald:
18 bali ni sisi tunaomtukuza Bwana, sasa na hata milele. Msifuni Bwana.
Maar wij, wij zullen Jahweh loven, Van nu af tot in eeuwigheid!