< Zaburi 114 >
1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
Quand Israël est sorti d'Égypte, la maison de Jacob d'un peuple de langue étrangère,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
Juda est devenu son sanctuaire, Israël sa domination.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
La mer le vit et s'enfuit. Le Jourdain a été repoussé.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
Les montagnes ont sauté comme des béliers, les petites collines comme des agneaux.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
Qu'est-ce qui t'a fait fuir, toi la mer? Vous, Jordan, vous avez fait demi-tour?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
Vous, montagnes, que vous avez fait sauter comme des béliers? Vous êtes des petites collines, comme des agneaux?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
Tremblez, terre, devant la présence du Seigneur, en présence du Dieu de Jacob,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
qui a transformé le rocher en une mare d'eau, le silex en une source d'eau.