< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
Alleluya. In the goyng out of Israel fro Egipt; of the hous of Jacob fro the hethene puple.
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
Judee was maad the halewyng of hym; Israel the power of hym.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
The see siy, and fledde; Jordan was turned abac.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
Munteyns ful out ioyeden as rammes; and litle hillis as the lambren of scheep.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
Thou see, what was to thee, for thou fleddist; and thou, Jordan, for thou were turned abak?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
Munteyns, ye maden ful out ioye as rammes; and litle hillis, as the lambren of scheep.
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
The erthe was moued fro the face of `the Lord; fro the face of God of Jacob.
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Which turnede a stoon in to pondis of watris; and an hard rooch in to wellis of watris.

< Zaburi 114 >