< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
When Israel went out of Egypt, Jacob’s house from a barbarous people,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
God chose Judah for himself, Israel became his kingdom.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
The sea saw it, and fled, Jordan river ran backwards.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
Mountains skipped like rams, hills like the young of the flock.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
Why, sea, do you flee? Jordan, why run backwards?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
Mountains, why skip ram-like? Why, hills, like the young of the flock?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
Earth, tremble before the Lord, at the presence of Jacob’s God,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
who turns rocks into pools of water, and flint into fountains of water.

< Zaburi 114 >