< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
When Israel came forth from Egypt, The house of Jacob from a people of strange language,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
Judah was his sanctuary, And Israel his dominion.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
The sea beheld, and fled; The Jordan turned back.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
The mountains skipped like rams, And the hills like lambs.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
What aileth thee, O thou sea! that thou fleest? Thou, Jordan, that thou runnest back?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
Ye mountains, that ye skip like rams, And ye hills like lambs?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
Tremble, O earth! at the presence of the Lord, At the presence of the God of Jacob;
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Who turned the rock into a standing lake, And the flint into a fountain of water!

< Zaburi 114 >