< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
When Israel came forth out of Egypt, the house of Jacob from a people of strange language;
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
Judah became His sanctuary, Israel His dominion.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
The sea saw it, and fled; the Jordan turned backward.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
The mountains skipped like rams, the hills like young sheep.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
What aileth thee, O thou sea, that thou fleest? thou Jordan, that thou turnest backward?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
Ye mountains, that ye skip like rams; ye hills, like young sheep?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
Tremble, thou earth, at the presence of the Lord, at the presence of the God of Jacob;
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Who turned the rock into a pool of water, the flint into a fountain of waters.

< Zaburi 114 >