< Zaburi 114 >
1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
When Israel went out of Egypt, the house of Jacob from a barbarous people:
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
Judea made his sanctuary, Israel his dominion.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
The sea saw and fled: Jordan was turned back.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
The mountains skipped like rams, and the hills like the lambs of the flock.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
What ailed thee, O thou sea, that thou didst flee: and thou, O Jordan, that thou wast turned back?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
Ye mountains, that ye skipped like rams, and ye hills, like lambs of the flock?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
At the presence of the Lord the earth was moved, at the presence of the God of Jacob:
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Who turned the rock into pools of water, and the stony hill into fountains of waters.