< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
當以色列出離埃及時,雅各伯家離開蠻夷時,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
猶大成了上主的聖所,以色列成了祂的王國;
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
海洋見了,頓時逃溜,約旦立即回轉倒流。
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
山嶽跳躍如公羊,丘陵舞蹈似羔羊。
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
海洋,什麼使您逃溜。約旦,什麼叫您倒流?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
山嶽,您們為什麼跳躍像公羊?丘陵,您們為什麼舞蹈似羔羊?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
大地,您應該在上主的面前,在雅各伯的天主面前搖撼,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
祂使磐石變為水潭,祂使礁石變成水泉。

< Zaburi 114 >