< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Хвалите, отроцы, Господа, хвалите имя Господне.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Буди имя Господне благословено отныне и до века.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
От восток солнца до запад хвально имя Господне.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Высок над всеми языки Господь: над небесы слава Его.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Кто яко Господь Бог наш? На высоких живый,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
и на смиренныя призираяй на небеси и на земли:
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
воздвизаяй от земли нища, и от гноища возвышаяй убога:
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
посадити его с князи, с князи людий своих:
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
вселяя неплодовь в дом, матерь о чадех веселящуся.

< Zaburi 113 >