< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Louvai ao Senhor. louvai, servos do Senhor, louvai o nome do Senhor.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Seja bendito o nome do Senhor, desde agora para sempre.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
Desde o nascimento do sol até ao ocaso, seja louvado o nome do Senhor.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Exaltado está o Senhor acima de todas as nações, e a sua glória sobre os céus.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Quem é como o Senhor nosso Deus, que habita nas alturas?
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
O qual se abate, para ver o que está nos céus e na terra!
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
Levanta o pobre do pó, e do monturo levanta o necessitado,
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
Para o fazer assentar com os príncipes, mesmo com os príncipes do seu povo.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
Faz com que a mulher estéril habite na casa, e seja alegre mãe de filhos. louvai ao Senhor.

< Zaburi 113 >