< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
سپاس بر خداوند! ای بندگان خداوند، ستایش کنید! نام او را ستایش کنید!
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
نام او از حال تا ابد متبارک باد.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
از طلوع آفتاب تا غروب آن، نام خداوند را ستایش کنید!
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
خداوند بر همهٔ قومها حکمرانی می‌کند؛ شکوه او برتر از آسمانهاست.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
کیست مانند یهوه، خدای ما، که در آسمانها نشسته است؟
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
او از آسمان بر زمین نظر می‌افکند
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
تا شخص فروتن و فقیر را از خاک بلند کند و سرافراز نماید
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
و او را در ردیف بزرگان قوم خویش قرار دهد.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
خداوند به زن نازا فرزندان می‌بخشد و او را شادمان می‌سازد. سپاس بر خداوند!

< Zaburi 113 >