< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Alleluia. Laudate pueri Dominum: laudate nomen Domini.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Sit nomen Domini benedictum, ex hoc nunc, et usque in sæculum.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
A solis ortu usque ad occasum, laudabile nomen Domini.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Excelsus super omnes gentes Dominus, et super cælos gloria eius.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Quis sicut Dominus Deus noster, qui in altis habitat,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
et humilia respicit in cælo et in terra?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
Suscitans a terra inopem, et de stercore erigens pauperem:
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
Ut collocet eum cum principibus, cum principibus populi sui.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
Qui habitare facit sterilem in domo, matrem filiorum lætantem.

< Zaburi 113 >