< Zaburi 113 >
1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Hallelujah! Lobet, ihr Knechte des HERRN, lobet den Namen des HERRN!
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Gepriesen sei der Name des HERRN von nun an bis in Ewigkeit!
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
Vom Aufgang der Sonne bis zum Niedergang sei gelobt der Name des HERRN!
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Der HERR ist erhaben über alle Heiden, seine Herrlichkeit ist höher als der Himmel.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Wer ist wie der HERR, unser Gott, der in solcher Höhe thront?
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
Der so tief heruntersieht, auf den Himmel und auf die Erde;
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
der den Geringen aufrichtet aus dem Staub und den Armen erhöht aus dem Kot,
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
daß er ihn setze neben Fürsten, neben die Fürsten seines Volks;
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
der die Unfruchtbare im Hause wohnen macht, daß sie eine fröhliche Mutter von Kindern wird. Hallelujah!