< Zaburi 113 >
1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Halleluja! Lobet, ihr Knechte des HERRN, lobet den Namen des HERRN!
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Gepriesen sei der Name des HERRN von nun an bis in Ewigkeit!
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
Vom Aufgang der Sonne bis zu ihrem Niedergang sei gelobt der Name des HERRN!
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Erhaben über alle Völker ist der HERR, den Himmel überragt seine Herrlichkeit!
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Wer ist dem HERRN gleich, unserm Gott, der da thront in der Höhe,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
der niederschaut in die Tiefe, im Himmel und auf Erden?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
Er hebt aus dem Staub den Geringen empor und erhöht aus dem Schmutz den Armen,
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
um ihn sitzen zu lassen neben Edlen, neben den Edlen seines Volks.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
Er verleiht der kinderlosen Gattin Hausrecht, macht sie zur fröhlichen Mutter von Kindern. Halleluja!