< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Louez Yah! Louez, vous, les serviteurs de Yahvé, louent le nom de Yahvé.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Que le nom de Yahvé soit béni, à partir de maintenant et pour toujours.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
Depuis le lever du soleil jusqu'à son coucher, Le nom de Yahvé doit être loué.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Yahvé est élevé au-dessus de toutes les nations, sa gloire au-dessus des cieux.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Qui est semblable à Yahvé, notre Dieu, qui a son siège en haut,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
qui se baisse pour voir dans le ciel et sur la terre?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
Il fait sortir les pauvres de la poussière, et soulève les nécessiteux du tas de cendres,
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
afin qu'il le mette avec les princes, même avec les princes de son peuple.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
Il installe la femme stérile dans sa maison. comme une joyeuse mère d'enfants. Louez Yah!

< Zaburi 113 >