< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Alleluya. Children, preise ye the Lord; preise ye the name of the Lord.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
The name of the Lord be blessid; fro this tyme now and til in to the world.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
Fro the risyng of the sunne til to the goyng doun; the name of the Lord is worthi to be preisid.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
The Lord is hiy aboue alle folkis; and his glorie is aboue heuenes.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Who is as oure Lord God, that dwellith in hiye thingis;
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
and biholdith meke thingis in heuene and in erthe?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
Reisynge a nedi man fro the erthe; and enhaunsinge a pore man fro drit.
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
That he sette hym with princes; with the princes of his puple.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
Which makith a bareyn womman dwelle in the hous; a glad modir of sones.

< Zaburi 113 >