< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Praise Yahweh! You people who serve Yahweh, praise him! Praise (him/his name)!
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Yahweh should be praised now and forever!
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
People who live in the east and people who live in the west, everyone, should praise Yahweh [MTY]!
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Yahweh rules [MTY] over all the nations, and high in the heavens he shows that his glory is very great.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
There is no one [RHQ] who is like Yahweh, our God, who lives/sits/rules in the highest heaven,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
and looks far down through the heavens and sees the [people on] the earth.
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
[Sometimes] he lifts poor people up [so that they no longer sit in] the dirt; he helps needy [people so that they no longer sit on] heaps of ashes
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
and causes them to [be honored] by sitting next to princes, the sons of the kings [who rule] their people.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
He also enables women who have no children to have a family; he causes them to be happy mothers. Praise Yahweh!

< Zaburi 113 >