< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Hallelujah. Praise the Lord, you his servants, praise the name of the Lord.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
The name of the Lord be blessed from now and for evermore.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
From sunrise to sunset is the name of the Lord to be praised.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
High is the Lord above all nations, above the heavens is his glory.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Who is like the Lord our God, seated on high?
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
He bends down to look at the heavens and earth.
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
He raises the weak from the dust, he lifts the poor from the dunghill,
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
and sets them beside the princes, even the princes of his people.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
He gives the childless woman a home, and makes her the happy mother of children. Hallelujah.

< Zaburi 113 >