< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Praise ye the LORD! Praise, O ye servants of the LORD! Praise the name of the LORD!
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Blessed be the name of the LORD From this time forth, even for ever!
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
From the rising of the sun to its going down, May the LORD'S name be praised!
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
The LORD is high above all nations; His glory is above the heavens.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Who is like the LORD, our God, That dwelleth on high,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
That looketh down low Upon the heavens and the earth?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
He raiseth the poor from the dust, And exalteth the needy from the dunghill,
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
To set him among princes, Even among the princes of his people.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
He causeth the barren woman to dwell in a house, A joyful mother of children. Praise ye the LORD!

< Zaburi 113 >