< Zaburi 113 >
1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Hallelujah. Praise, O ye servants of the Lord, praise ye the name of the Lord.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Let the name of the Lord be blessed from this time forth and for evermore.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
From the rising of the sun unto his going down the name of the Lord is praised.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
High above all nations is the Lord, above the heavens is his glory.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Who is like the Lord our God, who dwelleth on high?
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
Who condescendeth to view what is done in the heavens, and on the earth?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
He raiseth up out of the dust the poor, from the dunghill he lifteth up the needy:
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
That he may set him with princes, even with the princes of his people.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
He causeth the barren woman to dwell in the midst of [her] household, the joyful mother of children. Hallelujah.