< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Hallelujah. Praise, O ye servants of the LORD, praise the name of the LORD.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Blessed be the name of the LORD from this time forth and for ever.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
From the rising of the sun unto the going down thereof the LORD'S name is to be praised.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
The LORD is high above all nations, His glory is above the heavens.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Who is like unto the LORD our God, that is enthroned on high,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
That looketh down low upon heaven and upon the earth?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
Who raiseth up the poor out of the dust, and lifteth up the needy out of the dunghill;
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
That He may set him with princes, even with the princes of His people.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
Who maketh the barren woman to dwell in her house as a joyful mother of children. Hallelujah.

< Zaburi 113 >