< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Alleluia. Praise the Lord, children. Praise the name of the Lord.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Blessed is the name of the Lord, from this time forward and even forever.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
From the rising of the sun, even to its setting, praiseworthy is the name of the Lord.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
The Lord is high above all nations, and his glory is high above the heavens.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Who is like the Lord, our God, who dwells on high,
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
and who gazes upon the humble things in heaven and on earth?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
He lifts up the needy from the ground, and he urges the poor away from filth,
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
so that he may place him with the leaders, with the leaders of his people.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
He causes a barren woman to live in a house, as the joyful mother of sons.

< Zaburi 113 >