< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Hallelujah! Give praise, O servants of the LORD; praise the name of the LORD.
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Blessed be the name of the LORD both now and forevermore.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
From where the sun rises to where it sets, the name of the LORD is praised.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
The LORD is exalted over all the nations, His glory above the heavens.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Who is like the LORD our God, the One enthroned on high?
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
He humbles Himself to behold the heavens and the earth.
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
He raises the poor from the dust and lifts the needy from the dump
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
to seat them with nobles, with the princes of His people.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
He settles the barren woman in her home as a joyful mother to her children. Hallelujah!

< Zaburi 113 >