< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
¡Alaben al Señor! ¡Felices son los que lo respetan, quienes aman seguir sus mandamientos!
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
Sus descendientes prosperarán en la tierra prometida; los hijos de aquellos que hacen el bien serán prosperados.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
Sus familias serán ricas; porque el bien que ellos hacen tendrá resultados eternos.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
La luz brillará en las tinieblas para aquellos que viven en rectitud, para aquellos que son corteses, compasivos, y buenos.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
Las cosas buenas llegan a aquellos que son generosos con sus préstamos y que son honestos a la hora de hacer negocios.
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
Porque nunca caerán. Los que viven con rectitud nunca serán olvidados.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
No tienen miedo de las noticias que vengan porque confían completamente en Dios.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
Están seguros y son valientes, y ven a sus enemigos derrotados.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Comparten de forma generosa, dándole al pobre; el bien que hacen tendrá resultados eternos. Serán respetados grandemente.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Mas los impíos mirarán todo esto y se enojarán; rechinarán sus dientes con ira. Se consumirán, y todo lo que esperaban vendrá a ser nada.

< Zaburi 112 >