< Zaburi 112 >
1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
¡Hallelú Yah! Dichoso el hombre que teme a Yahvé, en sus preceptos halla el sumo deleite.
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
Su descendencia será poderosa sobre la tierra; la estirpe de los rectos es bendecida.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
En su casa hay bienestar y abundancia, y su justicia permanece para siempre.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
Para los rectos brilla una luz en las tinieblas: el Clemente, el Misericordioso, el Justo.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
Bien le va al hombre que se compadece y presta; reglará sus negocios con discreción;
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
nunca resbalará; el justo quedará en memoria eterna.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
No temerá malas nuevas; su corazón está firme, confiado en Yahvé.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
Su ánimo es constante, impávido, hasta ver confundidos a sus adversarios.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Distribuye y da a los pobres largamente; su justicia permanece para siempre, su triunfo será exaltado con gloria.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Lo verá el impío y se enfurecerá, se consumirá rechinando los dientes. Estéril será la envidia de los pecadores.