< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
Alleluja! Svētīgs ir tas vīrs, kas To Kungu bīstas, kam pie Viņa baušļiem labs prāts.
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
Tā dzimums būs varens virs zemes; taisno cilts taps svētīta.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
Padoms un bagātība ir viņa namā, un viņa taisnība pastāv mūžīgi.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
Taisniem tumsībā aust gaišums; jo Viņš ir žēlīgs, sirds žēlīgs un taisns.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
Labi tam cilvēkam, kas apžēlojās un aizdod, tiesā tas savu lietu vedīs galā.
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
Jo tas nešaubīsies ne mūžam; taisnais paliks mūžīgā piemiņā.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
No ļaunas slavas tas nebīstas viņa sirds ir stipra un paļaujas uz To Kungu.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
Viņa sirds ir droša un nebīstas; tiekams ar prieku skatās uz saviem pretiniekiem.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Viņš izdala un dod nabagiem; viņa taisnība paliek mūžīgi, viņa rags top paaugstināts ar godu.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Bezdievīgais to redzēs un apskaitīsies, viņš sakodīs savus zobus un iznīks; ko bezdievīgie kāro, ies bojā.

< Zaburi 112 >