< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
Alleluia. Beato l’uomo che teme l’Eterno, che si diletta grandemente nei suoi comandamenti.
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
Forte sulla terra sarà la sua progenie; la generazione degli uomini retti sarà benedetta.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
Abbondanza e ricchezze sono nella sua casa, e la sua giustizia dimora in perpetuo.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
La luce si leva nelle tenebre per quelli che son retti, per chi è misericordioso, pietoso e giusto.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
Felice l’uomo che ha compassione e presta! Egli guadagnerà la sua causa in giudizio,
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
poiché non sarà mai smosso; la memoria del giusto sarà perpetua.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
Egli non temerà alcun sinistro rumore; il suo cuore è fermo, fidente nell’Eterno.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
Il suo cuore è saldo, esente da timori, e alla fine vedrà sui suoi nemici quel che desidera.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Egli ha sparso, ha dato ai bisognosi, la sua giustizia dimora in perpetuo, la sua potenza s’innalzerà gloriosa.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
L’empio lo vedrà e ne avrà dispetto, digrignerà i denti e si struggerà; il desiderio degli empi perirà.

< Zaburi 112 >