< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
Louez l'Éternel! Heureux l'homme qui craint l'Éternel, Qui trouve tout son plaisir dans ses commandements!
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
Sa postérité sera puissante sur la terre; La race des hommes droits sera bénie.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
L'abondance et la richesse sont dans la maison du juste, Et sa justice demeure éternellement.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
La lumière se lève, même au sein des ténèbres, Pour l'homme droit, Pour celui qui est compatissant, miséricordieux et juste.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
Heureux l'homme compatissant. Celui qui prête aux malheureux: Il gagnera sa cause en justice;
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
Car il ne sera jamais ébranlé. La mémoire du juste vivra éternellement.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
Il n'a pas à craindre les bruits malveillants; Son coeur est ferme, plein de confiance en l'Éternel.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
Son coeur est inébranlable, inaccessible à la crainte: Il verra un jour la confusion de ses ennemis.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Il a distribué, il a donné ses biens aux pauvres; Sa justice demeure éternellement: Honoré de tous, il peut lever la tête.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Le méchant voit avec envie le bonheur du juste; Il grince des dents et se consume: Ainsi sont frappés d'impuissance les souhaits des méchants.

< Zaburi 112 >