< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
Halleluyah ·praise Yah·! א Blessed is the man who fears Adonai, בּ who delights greatly in his mitzvot ·instructions·.
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
גּ His offspring will be mighty in the land. דּ The generation of the upright will be blessed.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
ה Wealth and riches are in his house. ו His righteousness endures forever.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
ז Light dawns in the darkness for the upright, ח gracious, merciful, and righteous.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
ט It is well with the man who is merciful and lends. י He will maintain his cause in judgment.
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
כּ For he will never be shaken. ל The upright will be remembered forever.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
מ He will not be afraid of evil news. נ His heart is steadfast, trusting in Adonai.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
ס His heart is established. ע He will not be afraid in the end when he sees his adversaries.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
פּ He has dispersed, he has given to the poor. צ His righteousness endures forever. ק His horn will be exalted with kavod ·weighty glory·.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
ר The wicked will see it, and be grieved. שׁ He shall gnash with his teeth, and melt away. תּ The desire of the wicked will perish.

< Zaburi 112 >