< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
Praise the LORD. Blessed is the man who fears the LORD, who delights greatly in his commandments.
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
His descendants will be mighty in the land. The generation of the upright will be blessed.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
Wealth and riches are in his house. His righteousness endures forever.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
Light dawns in the darkness for the upright, gracious, merciful, and righteous.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
It is well with the man who deals graciously and lends. He will maintain his cause in judgment.
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
For he will never be shaken. The righteous will be remembered forever.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
He will not be afraid of evil news. His heart is steadfast, trusting in the LORD.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
His heart is secure, he has no fears; in the end he will look in triumph on his adversaries.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
He has scattered, he has given to the poor; his righteousness endures forever. His horn will be exalted with honor.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
The wicked will see it, and be grieved. He shall gnash with his teeth, and melt away. The desire of the wicked will perish.

< Zaburi 112 >