< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
Hallelujah! Blessed is the man who fears the LORD, who greatly delights in His commandments.
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
His descendants will be mighty in the land; the generation of the upright will be blessed.
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
Wealth and riches are in his house, and his righteousness endures forever.
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
Light dawns in the darkness for the upright— for the gracious, compassionate, and righteous.
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
It is well with the man who is generous and lends freely, whose affairs are guided by justice.
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
Surely he will never be shaken; the righteous man will be remembered forever.
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
He does not fear bad news; his heart is steadfast, trusting in the LORD.
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
His heart is assured; he does not fear, until he looks in triumph on his foes.
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
He has scattered abroad his gifts to the poor; his righteousness endures forever; his horn will be lifted high in honor.
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
The wicked man will see and be grieved; he will gnash his teeth and waste away; the desires of the wicked will perish.

< Zaburi 112 >