< Zaburi 112 >

1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
你们要赞美耶和华! 敬畏耶和华,甚喜爱他命令的, 这人便为有福!
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
他的后裔在世必强盛; 正直人的后代必要蒙福。
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
他家中有货物,有钱财; 他的公义存到永远。
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
正直人在黑暗中,有光向他发现; 他有恩惠,有怜悯,有公义。
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
施恩与人、借贷与人的,这人事情顺利; 他被审判的时候要诉明自己的冤。
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
他永不动摇; 义人被记念,直到永远。
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
他必不怕凶恶的信息; 他心坚定,倚靠耶和华。
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
他心确定,总不惧怕, 直到他看见敌人遭报。
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
他施舍钱财,周济贫穷; 他的仁义存到永远。 他的角必被高举,大有荣耀。
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
恶人看见便恼恨,必咬牙而消化; 恶人的心愿要归灭绝。

< Zaburi 112 >