< Zaburi 112 >
1 Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
亞肋路亞!凡敬畏上主的人,真是有福,喜歡他誡命的人,真是有福!
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
他的子孫在世上必要強盛,義人的後代必要受到讚頌。
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
他家中必有權勢財產,他的仁義必存留永遠。
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
上主富有仁愛慈悲公道,像光明在暗處向義人照耀。
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
樂善好施的人必蒙受祝福,祂以正義處理自己的事務。
6 Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
因為他永遠不會失足抖顫,義人必要受人永遠的記念。
7 Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
噩耗的凶信,不會使他驚慌,因為仰賴上主心志堅強。
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
直到看見他的仇敵蒙羞,他的心志堅強無懼無憂。
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
他散財周濟貧苦的人。他的仁義必萬世留存,他的頭角必受光榮。
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
罪人見到必要憤恨滿腔,咬自己的牙齒,焦灼難當,惡人的希望終必喪亡。