< Zaburi 111 >

1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Alleluya. Lord, Y schal knouleche to thee in al myn herte; in the counsel and congregacioun of iust men.
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
The werkis of the Lord ben greete; souyt out in to alle hise willis.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
His werk is knoulechyng and grete doyng; and his riytfulnesse dwellith in to the world of world.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
The Lord merciful in wille, and a merciful doere, hath maad a mynde of hise merueilis;
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
he hath youe meete to men dredynge hym. He schal be myndeful of his testament in to the world;
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
he schal telle to his puple the vertu of hise werkis.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
That he yyue to hem the eritage of folkis; the werkis of hise hondis ben treuthe and doom.
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
Alle hise comaundementis ben feithful, confermed in to the world of world; maad in treuthe and equite.
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
The Lord sente redempcioun to hys puple; he comaundide his testament with outen ende. His name is hooli and dreedful;
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
the bigynnyng of wisdom is the drede of the Lord. Good vndirstondyng is to alle that doen it; his preising dwellith in to the world of world.

< Zaburi 111 >