< Zaburi 111 >

1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Praise Yahweh! I will thank Yahweh with my entire inner being, every time I am with a large group of godly/righteous people.
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
The things that Yahweh has done are wonderful! All those who are delighted/pleased with those things desire to (study/think about) them.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
[Because of everything] that he does, people greatly honor him and respect him because he is a great king; the righteous/just things that he does will endure forever.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
He has [appointed/established festivals in which] we remember the wonderful things that he has done; Yahweh [always] is kind and merciful.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
He provides food for those who revere him; he never forgets the agreement that he made [with our ancestors].
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
By enabling his people to capture the lands that belonged to other people-groups, he has shown to [us], his people, that he is very powerful.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
He [MTY] faithfully [does what he has promised] and always does what is just/fair, and we can depend on him [to help us] when he commands us to do things.
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
What he commands must be obeyed forever; and he acted in a true and righteous manner when he gave us those commands.
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
He rescued [us], his people, [from being slaves in Egypt], and he made an agreement [with us] that will last forever. He [MTY] is holy and awesome!
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
Revering Yahweh is the way to become wise. All those who obey [his commands] will know what is good [for them to decide to do]. We should praise him forever!

< Zaburi 111 >