< Zaburi 111 >
1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Praise Yahweh - I will give thanks to Yahweh with all [the] heart in [the] council of upright [people] and [the] congregation.
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
[are] great [the] works of Yahweh [they are] studied by all [those] delighting in them.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
[is] splendor And majesty work his and righteousness his [is] enduring for ever.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
Remembrance he has appointed of wonders his [is] gracious and compassionate Yahweh.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
Food he gives to [those] fearing him he remembers for ever covenant his.
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
[the] power of Works his he has declared to people his to give to them an inheritance of nations.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
[the] works of Hands his [are] faithfulness and justice [are] reliable all precepts his.
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
[they are] sustained For ever for ever [they are] done in faithfulness and upright[ness].
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
Redemption - he sent for people his he ordained for ever covenant his [is] holy and to be feared name his.
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
[is the] beginning of Wisdom - [the] fear of Yahweh an understanding good [belongs] to all [those who] do them praise his [is] enduring for ever.