< Zaburi 111 >

1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Praise ye the LORD! I will praise the LORD with my whole heart, In the assembly of the righteous, and in the congregation.
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
The works of the LORD are great, Sought out by all who have pleasure in them.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
His deeds are honorable and glorious, And his righteousness endureth for ever.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
He hath established a memorial of his wonders; The LORD is gracious and full of compassion.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
He giveth meat to them that fear him; He is ever mindful of his covenant.
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
He showed his people the greatness of his works, When he gave them the inheritance of the heathen.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
The deeds of his hands are truth and justice; All his commandments are sure;
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
They stand firm for ever and ever, Being founded in truth and justice.
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
He sent redemption to his people; He established his covenant for ever; Holy, and to be had in reverence, is his name.
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
The fear of the LORD is the beginning of wisdom; A good understanding have all they who keep his commandments; His praise endureth for ever.

< Zaburi 111 >